Maandamano ya kumuunga mkono Imamoglu yazua vurugu Uturuki
2 Julai 2025Matangazo
Waziri wa mambo ya ndani wa Uturuki aliandika katika mtandao wake wa X kwamba watu hao 42 wanashutumiwa kumtusi rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan kushindana na maafisa wa usalama.
Maelfu ya watu waliandamana mjini humo kumuunga mkono meya Imamoglu ambaye amekuwa akiendesha kampeni ya upinzani dhidi ya serikali.
Uturuki yawakamata wapinzani wa Erdogan Izmir
Ekrem Imamoglu ni mwanasiasa mashuhuri nchini Uturuki anayekiongoza chama kikubwa cha upinzani cha CHP na anaangaliwa kama mpinzani mkubwa wa rais Erdogan katika chaguzi zijazo.
Alikamatwa na kuondolewa katika wadhifa wake Machi 23 huku maafisa kadhaa wa chama chake wakikamatwa.