MigogoroUkraine
Watu 31 wauawa Kiev kufuatia shambulio kubwa la Urusi
1 Agosti 2025Matangazo
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema kuwa mwezi uliopita wa Julai, Urusi iliishambulia Ukraine kwa kutumia droni 3,800 na karibu makombora 260.
Zelensky ametaja kuridhishwa na ukweli kwamba Marekani, mataifa ya Ulaya, na washirika wengine wanaona wazi na kulaani kile kinachotokea huku akisisitiza kuwa mashambulizi ya Urusi yanaweza kusitishwa ikiwa kutakuwepo juhudi za pamoja.
Hayo yanajiri wakati Ujerumani imesema leo kuwa itaanza hivi karibuni kuwasilisha kwa Ukraine mifumo miwili ya ulinzi wa anga ya Patriot iliyotengenezwa na Marekani.