MigogoroAfrika
Watu 27 wauwawa baada RSF kuuteka mji muhimu Sudan
3 Mei 2025Matangazo
Mji huo ni kituo muhimu kusini mwa jimbo la Kordofan magharibi unaotumiwa kuwapeleka wanajeshi Darfur magharibi mwa Sudan. Kwa mujibu wa Shirika la kufuatilia haki za binadamu la Emergency Lawyers wapiganaji wa RSF, waliwakamata raia hao na kuwauwa likiwashutumu kwa kushirikiana na jeshi rasmi la Sudan.
Soma zaidi: Takriban watu 542 wameuwawa Sudan ndani ya wiki tatu
Mapema Ijumaa, kundi hilo lilisema kuwa wapiganaji wake wameuteka pia mji wa wa El Khoei ulio umbali wa kilomita 100 kutoka En Nahud. Watu walioshuhudia wanasema wanajeshi waliondoka kwenye eneo hilo na kuelekea katika mji mkuu wa jimbo la Kordofan Kaskazini.