Watu 22 wauawa katika shambulizi la Israel, Gaza
16 Agosti 2025Matangazo
Kulingana na shirika hilo, takriban Wapalestina 13 waliouawa leo walipigwa risasi na wanajeshi wa Israel walipokuwa wakisubiri kupokea chakula cha msaada karibu na vituo vya usambazaji chakula kaskazini na kusini mwa ukanda huo.
Sheria mpya ya Israel yazidi kuzuia misaada Gaza
Msemaji wa shirika hilo Mahmud Bassal, amesema hali katika eneo hilo la Zeitun inazidi kudorora huku wakazi wakikosa kupata chakula na maji katikakati mwa mashambulizi ya Israeli.
Bassal pia amesema kuwa takriban watu 50,000 wanakadiriwa kuwa katika eneo hilo la Gaza City, wengi wakikosa bidhaa za kimsingi za maisha.