JamiiIndonesia
Watu 20 wapotea Indonesia kufuatia maandamano
2 Septemba 2025Matangazo
Maelfu ya Waindonesia waliingia barabarani katika maandamano ya kitaifa ya kupinga marupurupu makubwa kwa wabunge ambayo baadaye yaligeuka kuwa hasira kali ya umma dhidi ya polisi.
Machafuko hayo yalimlazimu Rais wa Indonesia Prabowo Subianto kubadili msimamo wake na kuchukua hatua ya kupunguza marupurupu ya wabunge lakini hatua hiyo haijafanikiwa kutuliza hasira ya umma.