MigogoroMashariki ya Kati
Watu 17 wauawa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel
29 Juni 2025Matangazo
Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji wa shirika la ulinzi wa raia la Gaza Mahmud Bassal. Jeshi la Israel liliwaamuru raia wa maeneo kadhaa ya Gaza kuondoka wakionya kuwa mashambulizi kadhaa yangelifanyika.
Jeshi la Israel limekataa kuzungumzia matukio hayo lakini limesema limekuwa likipambana ili "kuvunja uwezo wa kijeshi wa kundi la Hamas."
Hayo yakiarifiwa, Rais wa Marekani Donald Trump ametoa wito wa kufanikisha mazungumzo ya kusitisha vita vya Gazavilivyodumu kwa miezi 20. Duru zinasema Israel na Hamas wanakaribia kuyafikia makubaliano hayo.