Watu 15 wauwa katika shambulizi la Israel Gaza
15 Juni 2025Matangazo
Wafanyikazi katika hospitali za Al-Awda na Al-Aqsa katikati ya ukanda huo, waliripoti kuhusu tukio hilo na kusema watu walijeruhiwa.
Wanasema waathiriwa walikuwa raia wa kawaida waliokuwa wakijaribu kupata bidhaa hizo za msaada kutoka kwa wakfu wa
msaada wa kibinadamu wa Gaza (GHF).
Umoja wa Mataifa wapiga kura kutaka usitishaji mapigano Gaza
Hata hivyo, awali, ripoti hizo hazikuweza kuthibitishwa kwa njia huru.
Wakfu huo na jeshi la Israel pia hazikujibu maswali kuhusiana na hali hiyo.
Wakfu huo unaosimamiwa na Israel na Marekani, ulianza shughuli zake Gaza mwezi uliopita baada ya takriban miezi mitatu ya kizuizi cha Israel dhidi ya kuingizwa kwa misaada Gaza.