MigogoroMashariki ya Kati
Watu 14 wauawa Gaza huku misaada ikiendelea kutolewa
30 Julai 2025Matangazo
Kulingana na ripoti iliyoidhinishwa na Umoja wa Mataifa, watu wapatao milioni mbili wa ukanda wa Gaza unaokumbwa na vita vya karibu miezi 22, wanakabiliwa na viwango vikubwa vya njaa.
Rais wa Marekani Donald Trump ameahidi bila kutoa maelezo zaidi kuwa nchi yake itatoa msaada zaidi wa chakula na kutahadharisha kuwa watoto wa Gaza wanakufa njaa.
Mjumbe wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati , Steve Witkoff anatarajiwa hivi leo kuelekea Israel ambako atashiriki mazungumzo kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayoshuhudiwa huko Gaza.