SiasaBolivia
Wasoshalisti wapata pigo uchaguzi wa rais Bolivia
18 Agosti 2025Matangazo
Mshindani wake wa karibu ni rais wa zamani kutoka kambi ya wahafidhina Jorge "Tuto" Quiroga ambaye amejikingia asilimia 26.4 za kura. Matokeo hayo ni pigo kubwa kwa muungano wa chama tawala cha kisoshalisti cha MAS kilichozitawala siasa za Bolivia kwa zaidi ya miaka 20.
Mgombea wake Eduardo del Castillo ameambulia asilimia 3.2. Uchaguzi huo uliofanyika Jumapili ulitawaliwa na malalamiko makubwa kuhusu hali mbaya ya uchumi na kukosekana kwa mwanasiasa mashuhuri na rais wa zamani, Evo Morales, aliyezuiwa kugombea.
Kutokana na kukosekana mgombea aliyefikisha asilimia 50 ya kura, yumkini duru ya pili ya uchaguzi itaitishwa baadae mwezi huu.