UchumiMarekani
Wajumbe wa China na Marekani kujadili mzozo wa kibiashara
27 Julai 2025Matangazo
Mazungumzo hayo yanalenga pia kuendeleza makubaliano ya mwezi Juni ya kuzuia kwa muda Washington na Beijing kuwekeana ushuru mkubwa. China inatakiwa kufikia Agosti 12 kuwa imesaini makubaliano ya ushuru na utawala wa Rais Donald Trump.
Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Besent na Makamu Waziri Mkuu wa China He Lifeng ndio wataongoza mazungumzo hayo. Bila makubaliano hayo kuna hatari kwamba minyororo ya usambazaji wa kimataifa inaweza kukabiliwa msukosuko mpya kutokana na hatua ya ushuru inayoweza kufikia asilimia 100.