Raia wa Gabon wanapiga kura kumchagua Rais
12 Aprili 2025Matangazo
Uchaguzi huu ni muhimu kwa Gabon yenye jumla ya watu milioni 2.3, ambapo theluthi moja miongoni mwao wanaishi katika umasikini mkubwa licha ya utajiri mkubwa wa mafuta kwenye taifa hilo.
Soma zaidi: Gabon kufanya uchaguzi wa rais mwezi Aprili
Wachambuzi wa siasa wametabiri kuwa Rais wa mpito aliyehusika katika mapinduzi ya serikali iliyopita, Jenerali Brice Clotaire Oligui Nguema aliyetangaza kugombea urais mwezi uliopita, atashinda kwa kura nyingi. Itakumbukwa kuwa baada ya mapinduzi, Nguema aliahidi kurejesha mamlaka kwa raia kwa kufanya uchaguzi wa haki.