Wanamgambo wa Sudan watangaza kuunda serikali sambamba
28 Julai 2025Matangazo
Msemaji wa muungano wa Muungano huo wa Tasis, Alaa al-Din Naqd alitangaza mamlaka hiyo mpya kupitia taarifa kwa njia ya video kutoka mji wa Nyala ulioko eneo la Darfur linalodhibitiwa na RSF na washirika wake wa Janjaweed.
Muungano huo wa Tasis unaoongizwa na RSF, pia umemteuwa jenerali Mohamed Hamdan Dagalo, kamanda wa RSF kama mkuu wa baraza kuu katika utawala huo mpya.
Sudan yaishtumu Kenya kusambaza silaha kwa wapiganaji wa RSF
Mohammed Hassan al-Taishi, mwanasiasa wa kiraia ambaye alikuwa mwanachama wa baraza huru la kijeshi na kiraia ambalo lilitawala Sudan kufuatia
Kupinduliwa kwa al-Bashir mwaka 2019, ameteuliwa kuwa waziri mkuu katika serikali hiyo inayodhibitiwa na RSF.