MigogoroSudan
Wanamgambo wa RSF wawaua karibu raia 14
4 Agosti 2025Matangazo
Wanasheria wa Dharura wa makundi ya haki za binaadamu wanaofuatilia mzozo nchini humo wamesema watu wengine wengi walijeruhiwa na idadi kubwa wanashikiliwa kufuatia shambulizi la RSF siku ya Jumamosi kwenye viunga vya jiji la El Fasher, magharibi mwa Darfur.
Siku mbili kabla ya shambulizi hilo, uongozi wa RFS uliwataka wakaazi kuondoka Darfur na kwenda Qarni, ambako kulingana na wanasheria hao, ndio walikouliwa.
RSF imefanya shambulizi la hivi karibuni huko El-Fasher, ambao ni mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini lililozingirwa tangu Mei 2024.