MigogoroSudan
Kundi la RSF lauwa watu 40 katika kambi karibu na El-Fasher
12 Agosti 2025Matangazo
Mashirika ya kijamii yanayofanya kazi katika kambi hiyo inayowapa hifadhi watu wapatao 450,000, yamesema wapiganaji wa RSF walivamia na kuwalenga raia ndani ya nyumba zao.
Wanaharakati wa haki za binadamu katika mji huo wa el-Fasher unaodhibitiwa na jeshi, wamesema mashambulizi hayo yanadhihirisha kiwango cha kutisha cha ukiukaji unaofanywa na RSF dhidi ya watu wasio na hatia wala ulinzi wowote.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric ametahadharisha siku ya Jumatatu juu ya hali mbaya inayoendelea kushuhudiwa nchini Sudan.