RSF yashambulia kambi ya Abu Shouk Darfur Kaskazini
12 Agosti 2025Matangazo
Kundi la wanaharakati wa haki za binaadamu wanaotoa msaada kote nchini Sudan, limesema wanamgambo hao wanaopambana na jeshi la Sudan, wanasemekana kushambulia sehemu ya kambi hiyo na kuwalenga raia ndani ya nyumba zao.
Wanamgambo wa RSF wawaua raia 14 waliokuwa wakikimbia mapigano
Wanaharakati hao wamesema mashambulizi hayo yanadhihirisha kiwango cha kutisha cha ukiukaji unaofanywa na RSF dhidi ya watu wasio na hatia wala ulinzi wowote.
Awali msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric alitahadharisha juu ya hali mbaya inayoendelea kushuhudiwa nchini Sudan.