Wanajeshi wa akiba 50,000 wa Israel kuongezwa kwa vita Gaza
20 Agosti 2025Matangazo
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina kutokana na sheria za jeshi, afisa huyo amesema jeshi hilo litafanya shughuli zake katika sehemu za Jiji la Gaza ambako jeshi hilo bado halijafanya operesheni na ambako bado kuna shughuli nyingi za kundi la Hamas.
Hata hivyo afisa huyo amesema haijakuwa wazi ni lini operesheni hiyo itaanza.
Israel yataka mateka wote 50 waachiwe huru
Pia ameongeza kuwa takriban wanajeshi 50,000 wataitwa mwezi unaokuja, hatua itakayoongeza maradufu idadi ya maafisa hao wa akiba na kuifikisha hadi 120,000.
Tayari wanajeshi wa Israelwako Zeitoun na Jabaliya, vitongoji vya mji wa Gaza City ili kuandaa msingi wa operesheni hiyo iliyopanuliwa na ambayo inatarajiwa kuidhinsihwa na mkuu wa jeshi katika siku zijazo.