MigogoroAfrika
Wanajeshi 7 wa Uganda kutoka kikosi cha UN wauawa Somalia
23 Juni 2025Matangazo
Wanajeshi hao walikuwa sehemu ya Kikosi cha Umoja wa Mataifa Kusaidia Kuleta Utulivu nchini Somalia (AUSSOM) na kilichopewa jukumu la kupambana na kundi la kigaidi la Al-Shabaab na walipambana kwa muda wa siku tatu katika eneo la Lower Shabelle, na kufanikiwa kuukomboa mji huo mikononi mwa wanamgambo hao.
Mashambulizi ya hivi karibuni ya Al Shabaab yamezua hofu ya kuibuka tena kwa makundi ya itikadi kali katika taifa hilo la Pembe ya Afrika, hasa wakati huu kikosi cha AUSSOM kilichochukua nafasi ya kile cha ATMIS kikipambana na ukosefu wa askari wa kutosha pamoja na upungufu wa fedha.