MigogoroAfrika
Wanajeshi 5 wa Sudan Kusini wauawa na jeshi la Uganda
30 Julai 2025Matangazo
Hayo yameelezwa siku ya Jumatano na maafisa wa eneo hilo. Haijabainika wazi ni nini kilichochea mapigano hayo siku ya Jumatatu kati ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda (UPDF) na wanajeshi wa serikali katika Jimbo la Equatoria ya Kati, mapigano yaliyothibitishwa na Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF).
Uganda imekuwa ikihusika katika suala zima la usalama nchini Sudan Kusini, na kwa muda mrefu imekuwa ikitoa msaada wa kijeshi kwa Rais Salva Kiir, ikiwa ni pamoja na kutumwa kwa vikosi maalum tangu mwezi Machi mwaka huu.